Somo | Maelezo | Ada |
---|---|---|
![]() |
Kuchunguza Maandiko MatakatifuKozi hii inaeleza kifupi sehemu za Biblia na kusudi lake. |
0/- |
![]() |
Mungu Mmoja Njia MojaKwa mifano ya Agano la Kale na Agano Jipya kozi hii inaeleza jinsi Mungu alivyo na makusudi yake kwa watu wa dunia yetu. |
2000/- |
![]() |
Mtumishi wa MunguSomo hili linafafanua sehemu ya kitabu cha Injili ya Marko. |
2000/- |
![]() |
MunguKozi hii inachunguza maswali yafuatayo: |
2000/- |
![]() |
Neno la MunguSomo linahusu Injili ya Yohana, yaani kitabu cha nne cha Agano Jipya. Kinachoonesha habari ya Bwana Yesu na maisha yake duniani. Kinatueleza kuwa Yesu ni neno la Mungu na matendo yake aliyotenda. Somo hili likusaidie kumjua Mungu mwenyewe. |
2000/- |
![]() |
Njia ya WokovuJinsi ya kuupata wokovu wa Mungu ni jambo gumu linalowasumbua watu wengi sana leo. Kitabu hiki kinaeleza mambo muhimu yanayohusu jambo hili. |
2000/- |
![]() |
Chupa12Mtume Petro aliwaambia Wakristo kuwa lazima wawe kama watoto wachanga na siku zote wawe na kiu ya maziwa safi ya kiroho, |
2000/- |
![]() |
Majuma mawili katika Shule ya MaombiKwa mfano wa mtu na mchungaji wake tunajifunza jinsi ya kuzungumza na kumsikiliza Mungu. |
2000/- |
![]() |
Maisha ya MkristoMasomo ya kitabu hiki yanatufundisha baadhi ya mambo yaliyo muhimu sana katika maisha ya Mkristo. Lakini tutafakari maana ya maneno hayo Mkristo na Maisha. Biblia husema kwamba wanaomwamini Yesu Kristo wana “uzima wa milele,” milele maana yake daima. Mkristo akifa ataendelea kufurahia aina hii ya maisha katika nyumba ya Mungu, mbinguni. |
2000/- |
![]() |
Biblia IfunzavyoMafundisho ya msingi kuhusu Biblia, Mungu, dhambi, Wokovu n.k. |
2000/- |
![]() |
Mwokozi wa UlimwenguMaelezo ya Injili ya Luka. |
2000/- |
![]() |
Mwenendo wa mwaminiMatokeo ya kuzaliwa mara ya pili, uhakika wa wokovu, kushinda majaribu n.k. |
2000/- |
![]() |
Waraka kwa WarumiWaraka huu unaonesha jinsi Mungu anavyokutana na nia mbalimbali ambazo akili za mwanadamu huzifuata katika kuhusiana naye mwenyewe na kweli zake. |
2000/- |
![]() |
Je, Twaweza Kumjua Mungu?Watu wengi hawamwamini Mungu. Wengine huishi tu kana kwamba hakuna Mungu. Wengine husema, labda Mungu yupo lakini hakujionesha kwa wanadamu. Kwanza tutajibu swali lisemalo, “Je, kuna Mungu?” Pia maswali yafuatayo yatachunguzwa: Mungu yukoje? Mwanadamu ni nani? N.k. |
2000/- |
![]() |
Wanaume Waliokutana na BwanaKatika somo hili tumechagua wanaume sita waliokutana na Bwana Yesu katika matukio yaliyohusiana na kifo chake. Walifanya nini watu hao katika wakati huo muhimu? Ndiyo, baadhi yao walitenda kinyume naye; na wengine walimwunga mkono kwa ujasiri. Na sehemu ya yale waliyoyatenda na kuyasema, yameandikwa kwa ajili yetu kwamba tuweke moyoni mafunzo tunayopata humo. |
2000/- |
![]() |
Petro na KanisaMafundisho kufuatano na maisha ya Petro uhusiano wake na kanisa. |
2000/- |
![]() |
Kukua katika ImaniHatua zinazosaidia kukua katika Imani na umuhimu wake, k.m. kutubu, kukariri mistari ya Biblia, matendo mema n.k. |
2000/- |
![]() |
Roho Mtakatifu na Kazi YakeRoho Mtakatifu ni nani? Mifano ya kazi za Roho Mtakatifu na nguvu yake. |
2000/- |
![]() |
Biblia ni ya AjabuUmoja wa Biblia, Biblia ilitokeaje, Kanuni ya Biblia, kuenezwa kwa Biblia duniani. Biblia ni pumzi ya Mungu. |
2500/- |
![]() |
Nyaraka za YohanaNyaraka za Yohana ni za kiutendaji. Pia zinaweza kushtua, kwa sababu Yohana anazungumzia mambo yote kwa uwazi bila kuficha jambo lolote katika maisha yetu. Mambo hayo yote ama ni meupe au meusi, ni ya kweli au uongo, mema au maovu ameyataja. “Mungu ni nuru, na ndani yake hakuna giza hata kidogo”. |
2500/- |
![]() |
Safari katika BibliaSomo linaanza na mpango wa Mungu kwa uumbaji. Mpango wa Mungu kwa mwanamume na mwanamke wa kwanza hadi mpango wa Mungu kwa kanisa na hata kwa siku zijazo zinaelezwa na mengine mengi pia. |
2500/- |
![]() |
Mambo YajayoBwana Yesu aliwaambia marafiki zake mambo mengi yatakayotokea baadaye. Jambo moja zuri limeandikwa katika Yohana 14:3, “Nitakuja tena”. Yeye alikuwa anaondoka ili awatayarishie mahali na kuahidi kuja tena. Alitaka wawe pamoja naye huko mbinguni. Je, Bwana Yesu yuko wapi leo? Yuko mbinguni, anataka tuwe pamoja naye mbinguni. Sisi hatuwezi kuona njia inayoelekea mbinguni au kufika wenyewe pale, kwa hiyo aliahidi kurudi tena. Huu ni ukweli mkuu wa kwanza ambao inabidi tuufahamu: Bwana Yesu aliahidi kuja tena. Somo linachunguza mambo mengi zaidi kwenye Biblia kuhusu muda ujao. |
2500/- |
![]() |
Chakula cha BwanaSomo linafundisha kuhusu Ushirika wa Chakula cha Bwana na Pasaka, mifano na maana yake, kutimiza agizo, na jinsi ya kujiandaa kwa Ushirika |
1000/- |
![]() |
1 WakorinthoJe, kuwako kwa madhehebu kunaungwa mkono na Maandiko? Kwa sababu ya dhambi gani Mkristo anaweza kutengwa na kanisa lake? Je, ni haki kwa mwamini kumshtaki mwamini mwenzake mahakamani? Ndoa inapewa nafasi gani katika Agano Jipya? Kipawa cha kunena kwa lugha ni nini? Mwili wa ufufuo utakuwaje? |
3000/- |
![]() |
Kuzikwa kwa njia ya UbatizoUchunguzi wa ubatizo katika Agano Jipya na uhusiano wake na imani katika Kristo. |
1000/- |
![]() |
Timotheo na TitoNyaraka hizi za uchungaji zinafundisha maana ya kanisa la kibiblia, wajibu wa Wakristo, na jinsi inavyopasa kanisa litawaliwe. |
3000/- |
![]() |
Kristo alilipenda KanisaKozi hii itakusaidia kwa kuiruhusu Biblia izungumze yenyewe kuhusu swala hilo la Kanisa. |
2000/- |
![]() |
Uvuvi wa WatuMojawapo ya faida kuu za mwamini, yaani mfuasi wa Kristo, ni kuhusishwa na Mungu katika kazi muhimu ya kuwavua watu, yaani kuwavuta kwa Bwana Yesu Kristo waokolewe (Mithali 11:30). Kati ya mambo yatendwayo na wanadamu ni machache tu ambayo matunda yake yatadumu milele. Hakika mtu anayefanya kazi hiyo anajiingiza kwenye mambo ya milele, na thawabu yake itadumu milele (Danieli 12:3). |
2000/- |
![]() |
UfunuoTunaishi katika siku za maana sana. |
3000/- |
![]() |
Al-KitabKwa moyo mkunjufu tunakukaribisha kwa kozi hii ya Biblia. |
3500/- |
![]() |
Matendo ya MitumeKitabu cha Matendo kinatusimulia jinsi kanisa la kwanza lilivyolikabili Agizo Kuu la Bwana. Kinatuambia jinsi Injili ilivyoenea magharibi na hatimaye kuingia katika jiji la Rumi. Kitabu hiki kinasimulia juu ya watu na pia sehemu mbalimbali. Kinadhihirisha kanuni za mipango makini ya kupeleka injili katika pande zote za ulimwengu. |
3500/- |
![]() |
Jifunze Biblia NzimaMafunzo haya yanaeleza kwa muhtasari vitabu vyote vilivyomo katika Biblia. Mambo hayo yote yameoneshwa katika nyakati zake, mahali pake pamoja na maelezo mafupi. |
3500/- |
![]() |
Kitabu cha MwanzoKitabu cha Mwanzo ni msingi na mahali pa kuanzia ujumbe wa Neno la Mungu zima. Ukitaka kuelewa vitabu vyote vya Biblia inakupasa ujue kitabu cha Mwanzo. |
3500/- |
![]() |
Injili ya MarkoMarko aliandika Injili hii kwa ajili ya mtu wa kawaida. |
3500/- |
![]() |
Njia ya Kutoka na KuingiaKitabu cha Mwanzo kinaishia na habari ya kufa kwa Yakobo katika nchi ya Misri. |
3500/- |
![]() |
Safari JangwaniVitabu vya Hesabu na Kumbukumbu la Torati ni sehemu muhimu za Neno la Mungu. Kama ukielewa kitabu cha Hesabu na cha Kumbukumbu la Torati, utaweza kuelewa vizuri zaidi sehemu nyingi za Biblia. Pia utaelewa zaidi kuhusu Mungu pekee wa kweli. Pia somo hili linalinganisha mistari ya vitabu hivi na Agano Jipya na kueleza zinatokea wapi katika Agano Jipya na kwa tukio gani. |
3500/- |